ZITTO KABWE AIKANA NAMBA YAKE YA SIMU LIVE BAADA YA CHADEMA WENZAKE KUDAI NI GAIDI NA ACHUNGUZWE
Sasa nashawishika kuamini kuwa CHADEMA wana lao juu ya mipango ya kigaidi...
Jana
Mabere marando alitoa tamko lefu sana lenye namba za simu
kibao za watu mashuhuri akitaka mahakama ichunguze simu zao
ikiwemo ya Zitto Kabwe.....
SWALI LA KUJIULIZA:
-Kwanini Mabere Marando anatoa tamko muhimu kama hili bila kuhusisha viongozi wa juu kama Zitto?
-Matamko ya nini wakati kesi iko mahakamani?
-Kwanini
chadema inaendelea kulizungumzia hili swala nje ya mahakama huku
wanaharakati wa chadema kama Mwanakijiji wakiwa wameshaanzisha harakati
za kutaka kesi ifutwe kwa swala kuzungumziwa nje ya mahakama?
HUU NI UJUMBE WA ZITTO AKIKANUSHA KUHUSIKA NA UGAIDI
( HAPA AMEANZA KWA KUNUKUU SEHEMU YA RIPOTI YA MABERE:)
Ndugu waandishi wa habari;
Pili,
nitakwenda mahakamani kuwasilisha ombi maalum la kuomba amri ya
mahakama kuagiza makampuni ya simu za mkononi kuwasilisha mahakamani
statement za simu za watu kumi (10) ili kusaidia mahakama kutenda haki
na jamii kujua ukweli wa mambo haya.
Watu
ambao nitaomba mahakama itoe amri ya kuletwa taarifa zao simu na meseji
(sms) ni Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa nchini (TISS), Jack Zoka,
anayetumia simu Na. 255756809535, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Mwigulu Lameck Nchemba....
HUU NDO UTETEZI WAKE
Namba
hiyo iliyotajwa katika TAMKO imewahi kuwa namba yangu ya Simu. Namba
hii nimeacha kuitumia toka mwezi Juni/Julai mwaka 2012.
Hata
hivyo namba hii bado inaonekana kwenye business card yangu na kwenye
email zangu sehemu ya anuani. Namba hii haijawahi kuwa ya Zoka. Imewahi
kuwa ya Zitto Zuberi Kabwe peke yake. Namba hii haitumiki toka katikati
ya mwaka 2012.
Mambo
mawili muhimu:ama namba hii imewekwa kwa bahati mbaya kwenye tamko
tajwa au imewekwa makusudi kwa sababu maalumu zenye lengo la kutoa
ujumbe fulani kwa watu.
Kwa
namna namba hii ilivyochomekwa kwenye tamko hili ni dhahiri kuna
juhudi za kunihusisha na upuuzi huu wa ugaidi na unyama dhidi ya
binaadamu.
Napenda
kusisitiza kwamba, sihusiki kwa namna yeyote ile katika kuwaza, kupanga
au kutekeleza mipango yeyote ya kudhuru mtu ama kwa njia za kigaidi au
za kijinai.
Sihusiki
kwa namna yeyote ile kupanga mpango wowote ule wenye lengo la kuhusisha
chama changu na vitendo vyovyote vya kigaidi au kudhuru mtu yeyote
yule.
Juhudi
zozote zinazofanywa na maadui wa chama changu za kunihusisha na mambo
haya zitashindwa kwani siku zote ukweli huwa bayana.
Napenda kuweka wazi kwamba Mhariri wa Mwananchi ndugu Dennis Msacky ni rafiki yangu wa karibu sana.
Ninaamini
kabisa kwamba katika suala hili Dennis Msacky ni victim.Juhudi zozote
zile za kutaka kumgeuza 'victim' kuwa mtuhumiwa lazima zitashindwa tu
kwani siku zote HAKI hutamalaki.
Mtu
yeyote anayetaka kutumia urafiki wangu na Dennis Msacky kutaka
kujifurahisha kisiasa ajue kuwa furaha yake hiyo itakuwa ni ya muda
mfupi sana maana ukweli ukidhihirika atapata aibu kubwa sana.
Ni muhimu sasa mambo haya tuiachie mahakama itende haki.
No comments:
Post a Comment