Tuesday 3 September 2013

CHADEMA WAMKANA AFANDE SELE....WADAI HAWAJAWAHI MUOMBA AGOMBEE UBUNGE MOROGORO


Gazeti la Habari Leo la siku ya leo tarehe 2 Septemba lenye kichwa cha habari "Chadema kuzoa wasanii mastaa" pamoja na mambo mengine, mwandishi amemnukuu mmoja wa wasanii toka mkoa wa Morogoro akisema amewahi kuombwa na viongozi wa mkoa wa CHADEMA kugombea Ubunge. 

NAOMBA KUWEKA KUMBUKUMBU SAHIHI.
1. Mimi ndiye mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro, ninayeongoza Baraza la Uongoz la mkoa lenye wajumbe wa5 tu tangu mwaka 2009. 
2. Katika vikao vyetu vyote hukujawahi kuwepo kwa AGENDA ya kumuomba/ kumshawishi mtu yeyote kugombea nafasi yoyote. 
3. Hatujawahi kumuomba Afande Sele kugombea. Mbali na hilo hatujawahi hata kumuomba tu kujiunga na CHADEMA.  
  4. Kwa upande wa gazeti la Habari leo, naungana na kauli ya JB kwamba, kuna dalili za wazi kwamba habari hii imepikwa na mwandishi mwenyewe. 

Asanteni Makamanda.
PUUZENI TAARIFA HII Susan Limbweni Kiwanga

No comments: