Thursday, 20 February 2014

LORI LA MAFUTA LADONDOKA MLIMA SEKENKE NA KUUA WATU WANNE PAPO HAPO


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgsBEySegeotQ-nFjqOPBae8sDidXeTuT3ZB4YvlIJA0LJzIY74iqkya6JkhzCq_ihTu36MUZ4ty_OqP-m89rzKujBL4QshgFLAKrNSLq7OkyEwyM5nCDuMXmZZrR9GbZfJUyVZoW8cbvUb/s1600/se4.jpg
LORI la mafuta limeanguka jioni hii katika eneo la milima ya sekenke mkoani Singida na kuua watu wanne papohapo.
 
Chanzo cha ajali hiyo ni kufeli breki lori hilo kukamata moto wakati lilipokuwa linashuka milima hiyo. Shuhuda wa ajali hiyo, bwana Julius Chacha alipoongea na Dj Sek Blog amesema kuwa lori hilo lilipoacha njia lilipinduka na kuingia bondeni na kushika moto.
 
Akiendelea kuongea, shuhuda huyo alisema walishindwa kutoa msaada wowote kwa kuwa moto uliposhika ulikuwa mkubwa na hawakuwa na vifaa vya kuokolea. Watu wanne wamekufa papohapo kutokana na ajali hiyo.  Polisi walikuwa bado hawajafika eneo la tukio mpaka tunaondoka eneo la tukio.
 
Wanainchi wakiangalia Lori baada ya kuungua

Mabaki ya Lori hilo bada ya kuteketea kabisa na moto jioni hii

Baadhi ya wasafiri wakitazama lori lililongua jioni hii
 
 
Bonde la mlima sekenke linavyoonekana na baadhi ya miti imeunguaa
Hii ni njia ya mlima sekenke
Haya ni mabaki ya mwili wa mmoja ya watu walikuwam kwenye Lori hiloo
Moto ukimalizikia kwa mbaliii kama inavyoonekana
(Picha na DJ Sek Blog)

No comments: