![](http://4.bp.blogspot.com/-TY4PHQ84baQ/UwWT5l4DbII/AAAAAAAAsOU/4sxhfC2rgZ8/s400/1.jpg)
Kampuni ya mtandao wa Kijamii ya Facebook imesema kuwa itanunua mtandao wa mawasiliano ya ujumbe mfupi wa WhatsApp kwa kima cha dola bilioni 16, na nyongeza zaidi ya dola bilioni 3 zitakazolipwa waanzilishi wa mtandao huo pamoja na wafanyikazi wake.
Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi kuwahi kutekelezwa na Facebook hadi kufikia sasa.
WhatsApp
ni maarufu sana miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma
ya kutuma ujumbe mfupi wa simu yaani SMS. WhatsAp imeweza kuwasajili
zaidi ya watumiaji milioni 450.
Katika
taarifa, mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa mtandao
huo upo njiani kuwaunganisha watu bilioni moja jambo ambalo litaifanya Facebook
kuwa na thamani kubwa.
No comments:
Post a Comment