Monday, 20 May 2013

YANGA YAICHAPA SIMBA 2-0/ MASHABIKI BARANI AFRIKA WAFURAHIA MECHI KUPITIA SuperSport EAST 9


gooo
Yanga wakifurahia mojawapo ya magoli kutoka katika mechi hiyo. Picha kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog
Timu ya soka ya Yanga, jioni hii imewadhihirishia mashabiki wao na wapenzi wa soka barani Afrika kwamba msimu huu ulikuwa wao baada ya kuwachapa wapinzani wao wa jadi,Simba kwa jumla ya magoli 2-0 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mchezo ambao ulionyeshwa kote barani Afrika kupitia SuperSport East 9 ndani ya DStv.
947367_194414630710874_1792139584_n
Mashabiki wa soka nchini Tanzania na barani Afrika waliweza kuona mpambano huu wa watani wa jadi Live kupitia kwenye luninga zao kwenye  SuperSport 9 East ambao walirusha matangazo hayo moja kwa moja kutokea Uwanja wa Taifa.
Katika mchezo huo magoli ya Yanga yalifungwa na Didier Kavumbagu kunako dakika ya 5 ya kipindi cha kwanza na Hamis “Diego” Kiiza kunako dakika ya 63 ya kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo, Yanga inamaliza msimu wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 60, ikifuatiwa na Azam FC yenye 52 na Simba 45.Hii ni mara ya 24 kwa Yanga kutwaa taji la Ubingwa wa Soka Tanzania Bara. Hongera kwa Yanga!

No comments: