MGOMBEA Ubunge Jimbo la Kalenga kupitia CHADEMA, Grace Tendega, amemuwekea pingamizi mgombea mwenzake kupitia CCM, Godfrey Mgimwa, kwa kile kinachodaiwa kuwa si raia wa Tanzania.
Tendega
alichukua fomu ya kumwekea pingamizi hilo juzi wakati zoezi la
kusitisha fomu za wagombea ukiwa umefikia kikomo. Jana majira ya mchana
mgombea huyo alirudisha fomu ya pingamizi kwa msimamizi wa uchaguzi huo,
Pudensiana Kisaka.
Akizungumza
na waandishi wa habari mratibu wa kanda wa CHADEMA Nyanda za Juu
Kusini, Frank Mwaisumbe, alisema mgombea alimwekea pingamizi akidai kuwa
si raia wa Tanzania.
Mwaisumbe
alisema kuwa kielelezo kingine ni mgombea huyo kuleta baadhi ya
wadhamini ambao si wakazi wa Jimbo la Kalenga na si wapiga kura wa jimbo
hilo.
"Kielelezo
kingine ni tarehe ya uteuzi wa mgombea wa CCM kuwa batili, ambapo
ilitajwa kuwa tarehe 16 badala ya 18,"alisema Mwaisumbe.
Wakati
huo huo, Majira ilimtafuta msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kalenga kwa
simu ya kiganjani, Pudensiana Kisaka, ambapo alikiri kuwa ni kweli
mgombea amerudisha fomu ya pingamizi na kusema kuwa hawezi kutolea
maelezo yoyote kwa kuwa ndio kwanza taratibu zinafanyika.
Jitihada
za kumtafuta mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM Godfrey Mgimwa ili ajibu
tuhuma hizo ziligonga mwamba kutokana na kuwa na vikao vya chama na
viongozi.
No comments:
Post a Comment